DOZI YA KIJANA.

Familia moja walimpekeka mtoto wao marekani kusoma,yule kijana alipomaliza shule kwa bahati akapata kazi kule kwa hiyo akaendelea kuishi kule kwamiaka mingi akiwa anaongea na wazazi wake katika simu tu. Jamaa akaomba likizo aje kuwaona wazazi wake. Alipokubaliwa akawa anapita madukani kutafuta zawadi zakuwaletea wazazi wake. Katika pitapita madukani akakuta dawa yakupunguza uzee. Jamaa akaona bora awanunulie wazazi wake ambao walishaanza kuzeeka.kwa bahati kunamtanzania alikua anarudi huku siku ya pili, yule jamaa akaamua ampe ile dawa atangulie nayo ili atapofika awakute wamebadilika. Siku ikafika yule jamaa akasafiri kuja tanzania. Alipofika uwanja wandege akategemea mapokezi yanguvu. Lakini jamaa hakuwaona wazazi wake. Akawa anaangaza huku nahuko bila kuwaona. Pembeni akamwona binti anambadilisha mtoto nepi. Akamwambi"binti hujambo?" Binti akajibu. Jamaa akamwambia hujawaona wazee wawili maeneo haya? Yule binti akamwuliza kwani weunawatafuta wakinanani? Kijana akamwambia wazazi wangu mr na mrs fulani. Yule binti akahamaki "jamani mwanangu waoooo" yule jamaa akamwambia binti umechanganyikiwa? Yule binti akamjibu hapana mimi mama yako. Ile dawa uliotuletea tulipotumia tukawa vijana ila baba yako kazidisha dozi ndoi huyu karudi utoto nilikua nambadili nepi kajisaidia" jamaa akapigwa namshangao akazimia.

No comments:

Post a Comment

Comment here::

Related Posts Plugin for WordPress, Blogger...